Skip to main content




KUONGEZA MSAMIATI WA KISWAHILI


Uundaji wa Maneno
Lugha hukua na kubadilika kila wakati kulingana na maendeleo ya jamii. Kigezo kimojawapo cha kukua na kubadilika kwa lugha ni kuongezeka kwa msamiati. Ili msamiati uongezeke katika lugha sharti maneno mapya yaundwe.


Njia za Uundaji Maneno
Uundaji wa Msamiati hutokea kwa njia mbalimbali zifuatazo:
Kubadili mpangilio wa herufi.
Kuambatanisha maneno.
Kutohoa maneno ya lugha nyingine.
Uambishaji wa maneno.
Kufanikisha sauti, umbo, mlio na sura.


Kuunda Msamiati kwa kubadili Mpangilio wa Herufi


Neno hujengwa kwa vitamkwa au herufi. Neno jipya lenye maana tofauti huweza kuundwa kwa kubadili mpangilio wa neno lingine
Mfano
Neno lima, lina herufi l, i, m, a, herufi hizi huweza kujenga maneno kama mali, kumi,imla, mila.
Neno tua lina herufi t, u, a, herufi hizi zina weza kujenga maneno kama:- tatu, tua, viatu, tatua.


NJIA YA KUAMBATANISHA MANENO



Kuna njia tatu za kuambatanisha meneno


Njia ya kurudufisha au kukariri neno
Mfano; barabara, sawasawa, polepole, katikati, vilevile.


Njia ya uundaji wa Msamiati kwa kuunganisha maneno mawili tofauti
Nomino na Nomino
Punda + mlia unapata Pundamilia
Bibi + Shamba unapata Bibishamba
Afisa + Elimu unapata Afisaelimu
Mwana + Siasa unapata Mwanasiasa
Bata + maji unapata Batamaji

Kuunganisha kitenzi na Nomino/Jina
Changa + moto changamoto
Chemsha + bongo chemshabongo
Piga + mbizi pigambizi
Zima + moto zimamoto

Kuunganisha maneno mawili na kudondosha baadhi ya herufi
Mfano
Baraza la Kiswahili Tanzania BAKITA
Mzaliwa wa mahali Fulani MZAWA
Chama cha Mapinduzi CCM
Nyamamfu NYAMAFU




KUTOHOA MANENO KUTOKA LUGHA NYINGINE


Kila lugha na tabia ya kuchukua maneno lugha nyingine ili kukidhi mahitaji ya Msamiati. Maneno kutoka lugha nyingine yanapoteuliwa hubadilishwa kimatamshiili ya fuate kanuniza Kiswahili. Maneno yanayotoholewa kutoka lugha nyingine husanifishwa na asasi za lugha ya Kiswahili ndipo ya ruhusiwe kutumiwa rasmi.

Mfano


Neno la Kiswahili
Lugha ya Mwanzo
Neno Lililotoholewa

Shule
Kijerumani
Schule

Salama
Kiarabu
Salaam

Duka
Kihindi
Dukan

Karoti
Kiingereza
Carrot

Shati
Kiingereza
Shirt

Picha
Kiingereza
Picture

Papai
Kihispania
Papaya

Meza
Kireno
Mezi

Shukrani
Kiarabu
Shukran

Ngeli
Kihaya
Engeli

Ikulu
Kinyamwezi
Ikulu

Ng'atuka
Kizanaki
Ng'atuka

Ndafu
Kichaga
Ndafu








Kuunda Maneno kwa Njia ya Uambishaji wa Maneno


Hii ni njia ya kubandika viambishi awali na tamati kwe nyekiini. Ujenzi wa maneno hutokana na mzizi mmoja kuonesha maana tofauti ingawa maana zina husiana.
Mfano mzizi: -lim-.Tukipachika viambishi awali na tamati tunapata maneno kama lima, analima, walilima, kilimo, limiana,halitalimwa na ukulima.
Kufananisha sauti, sura au tabia


Mfano
Kengele - utokana na sauti ya kengele inapo pigwa
Pikipiki - hutokana na muungurumo wa pikipiki
Ndizi mkono wa tembo – Ndizi inayo fananishwa na mkono wa mnyama tembo
Chubwi - Jiwe au chura atumbukiapo katika kina cha maji.


Mazingira yanayoelezea Kuhitaji Maneno Mapya


Mabadiliko mengi yanatokea kila siku katika nyanja mbalimbali za kimaisha-mabadiliko ya kiuchumi, kisiasa, kisayansi na kiteknolojia. Katika mazingira kama haya, watu watahitaji kuwasiliana, lugha itahitaji kuunda maneno ili kuwasilisha dhana mpya zilizoibuka. Kwa mfano, maneno kama vile nywila, kisakuzi, udukuzi, puku, talakirishi n.k yameundwa ili kuwasilisha dhana za kiteknoljia kwa Kiswahili.




Undaji wa Maneno katika Miktadha mbalimbali


Mabadiliko ya kimaendeleo yanafanya lugha ihitaji maneno ya kuyafikisha na kutumiwa na jamii. Ili kukidhi mahitaji hayo, maneno mapya yanazuka. Maneno hayo yanaweza kuwa katika fani mbalimbali, kama vile sayansi na teknolojia, siasa, utamaduni na uchumi kulingana na mkondo wa maendeleo. Mfano wa msamiati ni kama vile fedha, ushuru, kumpyuta, ukoloni, hospitali, suruali n.k

Popular posts from this blog

UFAHAMU UFAHAMU WA KUSIKILIZA Ufahamu wa kusikiliza ni zaidi ya kusikiliza tu kile kilichosemwa; badala yake ni uwezo wa mtu kuelewa maana ya maneno anayoyasikia na kuweza kuhusiana nayo kwa namna fulani. Kwa mfano mwanafunzi anaposikiliza hadithi, ufahamu mzuri wa kusikiliza humsaidia kuielewa hadithi hiyo, kuikumbuka, kuijadili, na hata kuisimulia tena kwa maneno yake mwenyewe. Kujibu Maswali ya Habari Uliyosikiliza Ufahamu wa kusikiliza unahusisha michakato kadhaa katika kuelewa na kupata maana ya kile kinachozungumzwa. Michakato hii inahusisha: Kuelewa vizuri sarufi ya lugha ile inayozungumzwa Kuelewa vyema maana ya maneno ya mhusiaka anayezungumza Kuelewa sintaksia (muundo wa maneno) ya sentensi kwa namna zinavyowasilishwa. Katika ufahamu wa kusikiliza, msikilizaji hana budi kuzingatia mambo yafutayo: 1. Kuwa makini na kuelekeza akili yote kwa mzungumzaji ili kuweza kusikia kila anachokisema. 2. Kutilia maanani vidokezo vya maana ili kubaini iwapo msemaji an...
UENEAJI WA KISWAHILI ENZI ZA WAINGEREZA NA BAADA YA UHURU Ukuaji na Ueneaji wa Kiswahili katika enzi ya Waingereza Waingereza walipochukua koloni la Tanganyika kutoka kwa Wajerumani walikuta Kiswahili kimeimarika na kinatumika katika maeneo mengi ya nchi. Kwa kuwa nao walihitaji kutawala hawakupuuzia matumizi ya Kiswahili katika utawala wao japo hawakutumia Kiswahili kwa lengo la kukikuza lakini walijikuta wanakieneza na kukikuza bila ya wao kukusudia. Mambo waliyochangia Waingereza katika Ukuaji wa Kiswahili nchini Tanzania Waingereza walitumia Kiswahili kama nyenzo ya kusaidia shughuli zao za kiutawala. Hata hivyo kuna mambo waliyofanya waingereza yaliyosaidia kukua na kuenea kwa Kiswahili, mambo hayo ni kama yafuatayo: 1. Shuguli za Kiuchumi Shuguli za kiuchumi wakati wa Waingereza zilihusisha kilimo na biashara. Kwa upande wa klimo, Waingereza waliendesha kilimo cha mazao mbalimbali, na walitumia mfumo wa kuajiri vibarua kutoka sehemu mbalimbali za nchi. Vibarua h...
KUTUNGA KAZI ZA FASIHI ANDISHI UTUNGAJI WA MASHAIRI Utungaji/uandishi wa kubuni ni ule unatokana na hisia ambazo zinamsukuma mtunzi ili atunge kazi yake. Hisia zinaungana na wazo ambapo vitu hivyo vinamsumbua akilini na kumkosesha raha. Mwandishi wa kubuni anataka aliwasilishe wazo lake ili hadhira ifahamu kilichopo moyoni mwake. Mwandishi hukosa usingizi na hivyo hulazimika kuamka na kuandika kile kinachomsukuma akilini mwake. Mambo ya Kuzingatia katika Utungaji wa Mashairi Uandishi wa kubuni unamtaka mtunzi atumie milango yake ya fahamu kinagaubaga. Kuna milango ya fahamu mitano ambayo ni pamoja na: kuona, kunusa, kusikia, kuhisi, na kuonja. 1. Kuona: je, mhusika unayemfikiria kichwani mwako unamwonaje? Umbo lake ni la kuvutia au kuchusha? Je, macho yake yakoje – je ni ya golori au la? Ni makubwa au madogo? Je, ni mlemavu wa macho? 2. Kunusa: pua zako zinakufanya usikie harufu gani? Je, ni harufu mbaya au nzuri? Je, ni uvundo au marashi? Je, mhusika wako ananuka...
UANDISHI UANDISHI WA INSHA ZA KIADA Insha ni kifungu cha maandishi kilichoandikwa kutokana na mtazamo wa mwandishi katika kujadili juu ya mada fulani. Mwandishi anaweza kuandika kuipinga mada hiyo au kuishadidia mada hiyo. Kuna aina mbili za insha, insha za kaida (zisizo za kisanaa) na insha za kisanaa. Insha za kaida ni insha zinazotumia lugha ya kawaida kuelezea mambo mbalimbali katika jamii, mfano juu ya mazingira, uchumi, biashara, historia n.k. Muundo wa Insha za Kaida Katika uandishi wa insha, muundo wake unakuwa na vitu vifuatavyo: 1. Kichwa cha insha; kichwa cha insha hudokeza kile ulichokijadili katika insha yako. Kwa mfano: Madhara ya matumizi ya madawa ya kulevya n.k 2. Utangulizi; Mambo yaliyopo katika utangulizi ni pamoja na kutoa fasili ya maneno muhimu na kuelezea kwa muhtasari mambo ambayo utakwenda kuyajadili katika insha yako. 3. Kiini cha insha; katika kiini ndipo kuna maelezo ya kina juu ya kile unachokijadili katika insha yako, maelezo ...